Wednesday, December 4, 2019

Hakiki fani katika Ushairi wa Mashairi ya Chekacheka

Fani katika Ushairi wa Mashairi ya Chekacheka
Hakiki fani katika Ushairi wa Mashairi ya Chekacheka
MWANDISHI: THEOBALD A. MVUNGI
WACHAPISHAJI: EDUCATIONAL PUBLISHERS AND DISTRIBUTORS LTD.
MWAKA: 1995
MUUNDO
Mwandishi ametumia muundo wa tarbia, mashairi yake yote yamefuata muundo huu. Beti za mashairi yake zina mistari minne. Mengi ya mashairi yake, mistari imegawanyika katika vipande viwili yaani mistari ina vina vya kati na vya mwisho. Mfano katika shairi la “Mashairi ya “Ngulu”;
https://sdimg.blob.core.windows.net/images/ShuleDirect/21994/Original/Screen_Shot_2016-07-27_at_16.29.37_1469626201232.png
Pia katika baadhi ya mashairi yake ameyaumba katika kipande kimoja, yaani yana kina cha mwisho tu. Mfano ni mashairi kama vile ya“Dhahabu ya fahari”, “Utu umekuwa kima”,“Seng’enge”mfano katika shairi la“Utu umekuwa kima”
https://sdimg.blob.core.windows.net/images/ShuleDirect/21994/Original/Screen_Shot_2016-07-27_at_16.31.45_1469626326589.png
MTINDO
Mtindo aliotumia mwandishi ni mtindo wa kimapokeo kwani amezingatia vigezo vya vina na mizani katika utunzi wa mashairi yake. Mfano katika shairi la”“Tuambae ukasuku”
https://sdimg.blob.core.windows.net/images/ShuleDirect/21994/Original/Screen_Shot_2016-07-27_at_16.33.11_1469626418348.png
MATUMIZI YA LUGHA
·                     Tashibiha:“Mshairi jihadhari, usishikwe kama fimbo.” – “Tuambae ukasuku.”“Na wasiothaminiwa, wapimwao kama nyasi”- “Raia si mali kitu”“Mapenzi yasinadiwe, kama shati dukani” – “Penzi lisilo heshima”“Utaliwa kama pumba” – “Utaliwa kama pumba”“Kaburu si mtu hata, kwake sisi sawa punda” – “Utumwa huru”.“Pungufu akili yake, mla punje kama kuku” – “Tuambaeukasuku
·                     Tashihisi:“Mejaribu kujongea, ndege awe mkononi,Yeye juu hurukia, namuomba samahani.” – “Njiwa kiumbe mtini”“Moyo nimeshauri, lakini umekaidiMoyo kiburi hatari, mfanowe kama radiMoyo mefumbata shari, unayakwepa marudi,Moyo u mwilini mwangu, jirudi tuwe pamoja.” – “Moyo”Nipishe wewe senge’nge” – “Seng’enge”.“Kijiji kisichoringa” – “Mashairi ya Ngulu”.“Akili yamsaliti, kikongwe haoni kweli.”- “ Ni wapi ushauri?”
·                     Sitiari:“Mshairi awe Nyati”- “Tuambae ukasuku”“Sisi ni miamba gogo”- “Raia si mali kitu”“Ile chai kikombeni, rangi yake Mwafrika” – “Chai”.“Kwetu ulikuwa mama” – “Indira”“Utu umekuwa kima” – “Utu umekuwa kima”“Uroho umekujaa, watu mefanya kondoo” – “Utaliwa kama pumba”
Matumizi ya semi
·                     Misemo:“Fedha fedheha” – “Chanzo cha huo uozo”
·                     Methali:“Akishaoza samaki, busara ni kumtupa” – “Chatu mmeza matonge”
·                     Nahau:“Wabunge waote meno, wasivilambe viatu” –wawe na mamlaka– “Tuambae ukasuku”Mbinu nyingine za kisanaa
·                     Takriri:“Chai ninaipa hati, kwa kutukidhia haja,Chai imewekwa kati, kwetu sisi sote waja,Chai majani ya miti, hii miti yenye tija.” – “Chai”Neno“njiwa” limejirudia katika kila ubeti –“Njiwa”Neno “moyo” limerudiwa katika kila ubeti. – “Moyo”Neno “mauti” limejirudia katika ubeti wa kwanza – “Utaliwakamapumba”Neno “Ngulu” katika mashairi ya “Ngulu”.
Ujenzi wa Taswira

Matonge”- madaraka-“Mwinyi umewasha moto”Nyati”– watawala –“Tuambae ukasuku”“Mfugaji”– mwananchi – “Tuambae ukasuku”“Jiko”– madaraka “Kuna nini huko jikoni”“Chatu”– watawala –“Chatu mmeza matonge”“Chura”– mtu asiye na msimamo - “Chura umegundulika”

No comments:

Post a Comment

CHUO CHA UALIMU MONTESSORI-MTWARA

Uhakiki Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya

Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya Hakiki Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya MWANDISHI: TAASISI YA KISWAHILI, ZANZIBAR WACHAPISHA...