Tuesday, July 24, 2018

SELIMUNDU

SELIMUNDU/ANEMIA SELIMUNDU
·         Ni ugonjwa wa kurithi usioambukiza ambao seli nyekundu za damu huwa na umbo la mwezi mchanga au mundu.
Mgonjwa wa selimundu damu yake huwa na seli nyekundu za damu za duara na kiwango kikubwa cha seli nyekundu zenye umbo la mwezi mchanga(selimundu)
Selimundu hazina uwezo wa kubeba hewa oksijeni inayotumika mwilini
Dalili za anemia selimundu
·         Kuchoka sana na kuwa dhaifu
·         Kupatwa na kizunguzungu
·         Kupatwa na maumivu ya kichwa
·         Kupatwa na baridi kwenye viganja vya mikono na miguu
·         Rangi ya macho kuwa manjano
·         Maumivu mwili mzima
Tiba
·         Kubadilisha uboho (rojorojo inayojaza nafasi za katikati za mifupa) kutoka kwa mtu asiye na ugonjwa
·         Tiba hii ni hatari sana maana kuna hatari ya kupoteza maisha

·         Tiba nyingine ni kuongezwa damu,kupunguza maumivu na kutumia antibiotiki

No comments:

Post a Comment

CHUO CHA UALIMU MONTESSORI-MTWARA

Uhakiki Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya

Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya Hakiki Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya MWANDISHI: TAASISI YA KISWAHILI, ZANZIBAR WACHAPISHA...