Tuesday, July 24, 2018

HUDUMA YA KWANZA

HUDUMA YA KWANZA
Huduma ya kwanza nimsaada wa haraka anaopewa mtu aliyepata ajali au kuugua ghafla kabla ya kumpeleka hospitali.ni msaada anaopewa mgonjwa kabla ya kumwona daktari.mfano huduma ya kwanza kwa mtu aliyeungua na moto,huduma ya kwanza kwa mtu aliyeumwa na nyoka,huduma ya kwanza kwa mtu aliyekunywa sumu.lengo kuu la huduma ya kwanza ni kuokoa maisha ya mgonjwa.



Vifaa/vitu ndani ya kisanduku cha huduma ya kwanza
Kifaa/kitu
Kazi katika huduma ya kwanza
mkasi
Kukatia vitu kama kamba,kitambaa,pamba nk
pamba
Kuasafishia jeraha
Kufungia jeraha
Mipira ya mkononi
Kujikinga dhidi ya maabukizi kupitia uwazi wa majeraha kwenye mikono
dawa
Kutuliza maumivu.mf panado
Kuua bacteria kwenye jeraha
Maji safi na salama
Kusafishianjeraha
Kusafishia vifaa
plasta
Kufunika kidonda kidogo
bendeji
Kufunga jeraha kwa kuzungusha
wembe
Kukatia vitu

HUDUMA ZA KWANZA MBALIMBALI

Aina ya Huduma ya kwnza

1.Aliyeumwa na nyoka na wadudu wenye sumu kali.

Wadudu wenye sumu kali ni kama nge,nyigu, nyuki n.k
Dalili za mtu aliyeumwa na nyoka/mdudu mwenye sumu kali
                                I.            Kuonekana kwa Jeraha sehemu aliyoumwa
                              II.            Uvimbe sehemu aliyoumwa
                            III.            Kuhisi maumivu makali ya jeraha
                            IV.            Mwili kupatwa ganzi
                              V.            Kuishiwa nguvu
hatua
a.       Hakikisha mgonjwa ametulia,asihangaike wala kutembea tembea
b.      Mlaze chali na asiinue sehemu iliyong’atwa juu zaidi ya usawa wa moyo
c.       Ondoa vitu vilivyombana kama pete au nguo
d.      Funga kamba juu ya jeraha
e.      Muwahishe kituo cha afya
f.        Kama nyoka/mdudu aliyemng’ata yupo (amekufa) nenda naye kituo cha afya
Tahadhari
Ø  Usioshe sehemu iliyoumwa na nyoka/mdudu mwenye sumu kali
Ø  Usikate wala kunyonya sehemu iliyoumwa na nyoka/mdudu mwenye sumu kali
Ø  Usijaribu kumshika nyoka/mdudu mwenye sumu kali aliye hai
2.aliyezirai
Dalili za mtu aliyezirai
        I.            Kutokwa na jasho
      II.            Kutoweza kuitikia unachomuuliza
    III.            Kupotea uwezo wa kuona
    IV.            Mapigo ya moyo kwenda taratibu
      V.            Kutoweza kuinuka mahali alipo
    VI.            Kupumua kwa shida

Visababishi vya mtu kuzirai
·         Mshituko wa ghafla
·         Magonjwa
·         Ajali

Hatua
a.       Mlaze mgonjwa chali
b.      Muangalie mgonjwa kama anapumua
c.       Nyanyua miguu yake juu kama sentimita 30
d.      Ondoa vitu vilivyombana
e.      Weka kitambaa kibichi kwenye paji la uso wake
f.        Muwaishe kituo cha afya


3.Aliyeungua na moto


Hatua
a.       Tumia maji barid ya bomba kupooza jeraha
b.      Safisha na kausha jeraha
c.       Funika majeraha kwa bendeji au kitambaa safi
d.      Muwaishe kitua cha afya
4.alievunjika mfupa (mguu au mkono)
Vifaa
Kipande cha barafu,miti(mbao) mbili,kamba mbili na dawa za kupunguza maumivu

Hatua za kufuata
a.       Ondoa nguo sehemu ya jeraha ibaki wazi
b.      Weka barafu
c.       Funga mbao mbili(miti) zilizonyooka upande wa kulia na kushoto mwa mkono au mguu uliovunjika
d.      Muwaishe kituo cha afya
5.mtu aliezama majini
Mazingira hatarishi  ya kusababisha kuzama majini
·         Kucheza kwenye mito mirefu,visima na madimbwi
·         Shughuli za uvuvi
·         Kuvuka mito mikubwa kwa miguu
·         Kuogelea kwenye kina kirefu
·         Kuogelea wakati wa mvua
·         Kuchota maji bila uangalifu kwenye visima virefu
Hatua za kufuata/kutoa huduma ya kwanza
a.       Hakikisha unajua kuogelea na mtoe ndani ya maji haraka sana
b.      Mlaze chali na msaidie kupumua kwa kumbonyeza tumbo kwa uangalifu na kuachia
c.       Gandamiza tumbo taratibu na mwinue atapike maji yaliyo katika mapafu
d.      Mpeleke muhusika hospitalini
6.mtu aliekunywa sumu
Tahadhari ya uhifadhi wa sumu na bidhaa za sumu        
·         Sumu/Bidhaa ya sumu iwe katika kifuko/chupa yake husika yenye kibandiko.
·         Sumu/Bidhaa ya sumu iwekwe kwenye kabati droo za juu na zifungwe kabisa
·         Sumu/Bidhaa ya sumu irudishwe sehemu husika baada ya matumizi
·         Vyombo vilivyotumiwa na Sumu/Bidhaa ya sumu visafishwe kwa maji mengi sa sabuni
·         Chupa na vifuko vyenye Sumu/Bidhaa ya sumu vilivyotumika  vichomwe haraka.
Hatua za kufuata / kutoa huduma ya kwanza
a.       Kama mgonjwa anajitambua muulize sumu gani amekunywa na mda gani kwa taratibu
b.      Mnyweshe maziwa mabichi kama yatapatikana haraka
c.       Kama mgonjwa hajitambui angalia kama anapumua
d.      Kama aina ya sumu ipo karibu basi soma kibandiko au ichukue.
e.      Muwaishe kituo cha afya.

No comments:

Post a Comment

CHUO CHA UALIMU MONTESSORI-MTWARA

Uhakiki Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya

Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya Hakiki Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya MWANDISHI: TAASISI YA KISWAHILI, ZANZIBAR WACHAPISHA...