Tuesday, July 24, 2018

VIUMBE HAI

VIUMBE HAI
Muundo na sifa za viumbe hai
Seli
Seli ni kiini cha msingi wa kiumbe hai.seli ni vitengo vya msingi vya uhai.
Mfano seli ya mimea,seli ya wanyama,seli ya bakteria nk
Aina za seli
       I.            Prokarioti
    II.            Eukarioti
Prokarioti ni aina ya seli ambayo haina utando wa nyukilia/kiini
Mf.seli ya bakteria
Eukarioti  ni aina ya seli yenye utando wa nyukilia/kiini.mf seli ya mnyama na seli ya mmea
Muundo wa seli za mnyama na mmea
Seli huundwa na sitoplazimu,kiwambo cha seli,nyukilia,vakuoli,kloroplasti na ukuta wa seli.kloroplasti na ukuta wa seli zipo kwenye seli yam mea tu.







sehemu ya seli
kazi
1.sitoplazimu
Ø  Ni kimiminiko kizito
Ø  Nyukilia,vakuoli na kloroplasti huelea katika sitoplazimu
·         Hutumika kama makazi ya nyukilia,vakuoli na kloroplasti
·         Mabadiliko ya kikemikali hutokea kwenye sitoplazimu

2.kiwambo cha seli
Ni kiwambo ambacho kimezunguka sitoplazimu kwa nje

·         Huruhusu vitu kuingia na kutoka kwenye seli.mf hewa,maji,vyakula na taka mwili

3.nyukilia
Imezungukwa na sitoplazimu (kiwambo cha nyukilia).

·         Hutawala na kuratibu shughuli zote za seli

4.vakuoli
Zina myeyuko angavu

·         Hutunza maji kwa mmea
·         Hutunza chakula
·         Husafirisha taka mwili kutoka kwenye seli

5.kloroplasti
Ni chembe ndogo sana zenye klorofili.klorofili huwa na rangi ya kijani ambazo hunasa mwanga wa jua ili kutengeneza chakula chake katika kloroplasti.
6.ukuta wa seli
·         Kutengeneza chakula cha mmea



·         Huzunguka seli ya mmea kwa nje
·         Kazihuipa seli umbo maalumu
·         Hulinda seli


Tofauti ya muundo kati ya seli ya mnyama na seli yam mea
Seli ya mnyama
Seli ya mmea
       I.            Haina ukuta wa seli
    II.            Haina kloroplasti
 III.            Ina vakuoli ndogo sana nay a muda mfupi
 IV.            Haina umbo maalumu
Ina ukuta wa seli
Ina kloroplasti
Ina vakuoli kubwa ya kudumu
Ina umbo maalumu



Viumbe hai
Ø  Ni vitu vinavyoonesha tabia na sifa zote za uhai kwa kiumbe.mf. binadamu,bakteria,mimea nk
Sifa za viumbe hai
1.      Huzaa na kuongezeka idadi
2.      Hujongea
3.      Hula chakula
4.      Hutoa taka mwili
5.      Hupumua
6.      Huhisi mabadiliko katika mazingira
7.       Hukua au kuongezeka kimo
Sifa za mimea
·         Mimea imendwa na seli nyingi
·         Hujitengenezea chakula
·         Seli na ogani mpya hutengenezwa kwenye ncha za mmea
·         Ina seli zenye ukuta wa seli
·         Hujilinda bila kujongea
·         Mimea ni eukarioti (seli zake zina kiini)
·         Mimea haijisogezi toka sehemu moja kwenda nyingine
·         Huhifadhi chakula kama wanga
Sifa za wanyama
·         Wanyama wameundwa kwa seli nyingi
·         Hawajitengenezei chakula
·         Seli zao hazina ukuta wa seli
·         Wanyama ni eukarioti
·         Wanyama hujisogeza sehemu moja kwenda nyingine
·         Huzaliana kwa kujamiana
·         Huhifadhi chakula kama glykojeni
Tofauti kati ya sifa za mimea na wanyama
Mimea
wanyama
Haina uwezo wa kujisogeza
wana uwezo wa kujisogeza
Hujitengenezea chakula
Hawajitengenezei chakula
Hutoa oksijeni nje na kupokea kabondaioksaidi
Hupokea oksijeni na kutoa kabondaioksaidi
Seli zao zina ukuta wa seli
Seli zao hazina ukuta wa seli
Huhifadhi chakula kama wanga
Huhifadhi chakula kama glykojeni

Mahitaji muhimu kwa uhai na ukuaji wa wanyama na mimea.
1.mahitaji muhimu kwa wanyama
a) Chakula
b) Hewa
c) Joto la wastani
d) Malazi
2.mahitaji muhimu kwa mimea
a) Mwanga wa jua
b) Maji
c) Hewa
d) Joto la wastani
e) Madini

f) Virutubisho 

No comments:

Post a Comment

CHUO CHA UALIMU MONTESSORI-MTWARA

Uhakiki Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya

Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya Hakiki Fani katika Ushairi wa Malenga Wapya MWANDISHI: TAASISI YA KISWAHILI, ZANZIBAR WACHAPISHA...